Afisa habari wa Simba sc Aji Manara amekutana na waandishi wa habari leo Jumamosi march 3,2018 kazungumzia mambo mbalimbali yanayohusu mchezo wao wa Caf Confederation Cup dhidi ya Al Masry unaotarajiwa kuchezwa siku ya Jumatano Machi 7,2018.
Miongoni mwa mambo aliyozungumzia Aji Manara ni viingilio, waamuzi, pamoja na maandalizi ya Simba Sc kuelekea mchezo huo na Al Masry.
Amesema mechi hiyo itachezwa kuanzia saa 12:00 jioni uwanja wa taifa, Manara amesema wamepanga muda huo kwa sababu mechi itachezwa siku ya kazi hivyo muda huo utakuwa rafiki kwa wadau wote.
Tumeweka viingilio vya aina tatu, mzunguko pamoja na Orange kiingilio itakuwa ni Tsh. 5000, VIP B Tsh. 15,000 na VIP A Tsh. 20,000.
Kuanzia keshokutwa vituo vyote vya Puma na sehemu nyingine zote ambazo nitazitaja kesho zitauzwa tiketi na watu wa Selcom kama ilivyo dasturi. Tutajitahidi kuwe na centre nyingi ili watu wapate tiketi kwa urahisi.
Klabu ya Al Masry itawasili kesho (Jumapili) jioni saa 12, siku ya Jumatatu jioni wafanya mazoezi kwenye uwanja wa taifa kama kanuni zinavyotaka kwa sababu Jumanne kutakuwa na mchezo wa klabu bingwa kati ya Yanga dhidi ya Township Rollers.
Waamuzi watawasili siku ya Jumatatu saa 10 jioni kutoka Afrika Kusini lakini mechi kamishna anatoka Elitrea ambaye atawasili siku moja pamoja na waamuzi.
Maandalizi mengine ndani ya timu yetu yanakwenda vizuri, timu imeingia kambini leo baada ya mchezo wa jana wa ligi kuu.

No comments:
Post a Comment